Patastories ni blog yenye kukupatia habari mbalimbali kwa njia ya picha zikiwemo za vijijini na mjini, karibu tujumuike pamoja.
Nitumie email: mnambajohn@gmail.com
Pichani ni majengo mapya ya Hospitali ya wilaya ya Tandahimba (Mtwara) yakiwa katika hatua ya mwisho kabisa. Kazi kwao wananchi siku za usoni kuyatunza.
Pichani sikuweza kuwapata wote ila ni baadhi ya vijana wakiwa chini ya mti majira ya saa tatu asubuhi. Hii nimeishuhudia sana vijijini mkoani Mtwara kwa vijana kulundikana vijiweni wakati wa kazi. Sio kwamba ardhi haipo ya kujishughulisha! Hapana jibu ni ipo, hiyo ndio hali kalisi.
Pichani ni bwawa lililopo kilomita kadhaa toka katikati ya wilaya ya Tandahimba (Mtwara), lipo njia iendayo kijiji kimoja kinaitwa Lyenje ambapo linapo jaa hutumiwa na wananchi walio karibu na eneo hilo hasa wakati wa shida ya maji. kwa sasa limekauka.