Saturday, January 31, 2009

Kwa wapenda Magari...

Link ifuatayo chini inaweza kukupa idea fulani kuhusu gari yako...

Fm Academia ndani ya Mtwara

Wazee wa Ngwasuma wakianza shughuli nzima.
Hizi zote ni mbwembwe kuwakonga wadau ukumbini.

Palikuwa hapatoshi.


Wadau na wapenzi wa Ngwasuma hawakuwa nyuma.

Ni full shangwe na Ngwasuma.





Teknolojia...

Teknolojia moja inapoipiku ingine huua kwa namna moja ama soko wa iliyopita, pichani ni kifaa chenye uwezo kama flash disk kenye uwezo wa kuhifadhi na kusikiliza mziki uwapo garini. Ni teknolojia nzuri sikata, hasa kwa barabara za vijijini ambapo CD kwenye kashkash za rafu road inakata kuimba. Wanasema Mchina huyo bwana.

Kijiweni...

Kwenye majengo wanapopangisha wanalipa kodi, je hapa napo vivyo hivyo? Swali.

Friday, January 30, 2009

Na hili je?

Unapoletewa maji kama haya je mara zote unakuwa na uhakika yanapotoka?
Au tunaangalia shida ilivyotubana tu...?

Cheka Kiafya!!

Add ImageKuna sehemu moja Mkoani Mtwara inaitwa Nakapanya na ingine inaitwa Nanguruwe, hii ni kweli na ucheke kiafya tu sio sana. Kuna dada mmoja wakati mahojiano yakiendelea kuhusu maisha yake nk, nk, ilifika kipindi katika maelezo yake ilikuwa hivi:
...mimi niliolewa Nakapanya nikaachika nikaenda kuishi Nanguruwe...
Yaani akimaanisha aliwahi ishi maisha ya ndoa Nakapanya na baadae akaenda kuishi Nanguruwe.
Ni story ya kweli si ya kutunga.
Kiafya tafadhali!

Ni mapambo tu sio wa ukweli.

Anaweza kuwa kivutio kama ni nyumbani kwako, garden nk nk.



Usafiri wetu kijijini ndio huooo!!

Hali ndio kama hivyo pichani, ukikosa Land Rover almaarufu Muhogo basi utapanda Kenta ama Lori. Ya mjini mjini na kijijini kijijini tu.

Hali halisi kipindi cha mvua...

Watoto hawa nimewakuta wakicheza kwenye maji yaliyotuama ya mvua. Yawezekana shida ya maji vijijini hufanya mpaka hali kama hii ikitokea watoto hawa husherekea. Na wazazi wao sio kwamba walikuwa mbali na watoto hao? Hapana.
Huyu ndie nisema kama kwenye swimming pool basi ndio yupo deep.
Vijimamboz hivyo na patastories.


Mambo yanapokwenda mrama!


Tairi la Lori aina ya fuso likiwa limechomoka na kubakiza nafasi ya fundi kuja kupata ugali wa watoto. Sijajua ni mzigo ulikuwa mzito ama vipi?

Ujenzi huu wa bila mifereji ya maji???

Pichani ni kwamba mkandarasi alipewa kipande cha kukikarabati, lakini kiukweli mifereji ja maji hamna na ndio sababau ya hali kama hiyo pichani. Comment!!

Ukweli kuhusu Prison Break

Prison Break

Ukweli kuhusu Prison Break, imezoeleka masikioni na machoni mwa wengi kuona mitaani Prison Break inapatikana mpaka season eight (8). Hii nathibitisha wazi kuwa Prison Break kihalisia haijafika season eight (8). Hizi mnazoziona mitani ni Episodes tu toka season halali season four (4).

Kwa wanaofuatilia kwa makini watajua ninamaanisha nini. Ukweli ni kwamba kibiashara tu ili kupata pesa wadau Fulani fulani ili wasilale njaa ndio wameamua kuikata kata vipande “episodes” hizo na kuzigawanya katika mafungu wayajuayo wenyewe na kuyaita “season Fulani mpaka Fulani. Ukweli unabaki pale pale kuwa wananchi wamekuwa wakinunua season moja mara nne zaidi bila wao kujua. Ila kutokana na utamu wa sinema yenyewe then watu kwao ni sawa tu bora kuona.

Ilikuwa ni katika kupeana dodoso tu habari ndio hiyo ipo nje nje.


Thursday, January 29, 2009

Ukisikia mkonge ndio huu!!!

Kama inavyoonekana pichani, mkonge wa moja ya gari za kazi Land Cruiser ukiwa umechomewa kwa lengo kuubwa la kupambana na vibaka. Inasemekana gari kama hiyo pindi (Mfano) ipatapo ajali wale wapenda kung'oa vifaa hukimbilia huo mkonge. Habari zinasema kwamba unagharama kuubwa sana ndio sababu ya vibaka kuwinda ulaji huo wanaojua/fahamu magari wanaelewa hilo.

Haya ndio mamboz ya vijijini (Biashara matangazo)


Ufahamu!!

Taa hii inatumia nishati ya umeme wa jua kwa kidhungu Solar power, pamoja na udogo wake inatoa mwanga wa kutosha kama tubelight tulizozizoea majumbani na kwingineko

Football ground.

Pichani unauona uzio ambao upende wa pili kuna mechi ikiendelea wakati picha hii inachukuliwa, kiingilio ndio kitachokuwezesha kujua ya upande wa pili.

Kama mweleka vile...!

Unaweza ukajua nini kimeikumba pikipiki hii?

Kijijini nako kweeema kabisa!

Na njiwa nae yupo kutafuta chakula pichani.

Kwa wengine hili ni "deal" au sio?


Kwenda kwa Rais mstaafu awamu ya tatu...

Unatambaa na mkeka saafi kabisa kwenda kijijini Lupaso (Masasi-Mtwara)
Kituo cha afya kijijini Lupaso hakipo nyuma.

Majengo ya Kitua hicho cha afya Lupaso karibu kabisa na kwa Mheshimiwa rais Mstaafu.



Enzi hizi hata mimi nilipita!!


Nauli!

Inasemekana kuwa kwa baadhi ya magari almaarufu makenta ama malori yabebayo abiria yanayofanya safari zake kwenda Tunduru kupitia njia ya Mtwara wanawake ndio hulipa nauli kubwa, hili nikauliza na kujibiwa kuwa baadhi ya makenta/malori hayo ni vimeo (Mabovu) hivyo linapohitaji msaada wa kulisumkuma liwake wanaume ndio wanashughulika. Swali je kwa mwanaume akitaka kulipa nauli kubwa kidogo na yeye atakubaliwa?

Wednesday, January 28, 2009

Comment!!!


Kutoka maktaba

Jumba la maajabu Zanzibar! Pembezoni kabisa mwa Forodhani ya zamani, kwa sasa forodhani ipo katika mchakato wa mwisho mwisho kakamilika pawe pa kisasa zaidi.

Mawaziri wa baadae hao!

Wakati mtoto wa kijijini kushika muhogo na kuutafuna mbichi mbichi ni kawaida, wa mjini analilia nya kwenye pakti... Maisha hayafanani kabisa.

Mambo ya patastories hayo!


Kukuz


Hii kali...

Dada hapo yupo bize kuisaini kijistika ndogo kwa ajili ya kumpatia mteja anaekuja kuacha simu yake kwaa ajili ya kuichaji, hii yote kuepukana na mafisadi wa simu wataodai kuwa waliacha za kwao zikichajiwa. Mambo ya kijijini hayo, tembea uone.

Stand ya Mabasi Masasi (Mtwara)


Bajaji, pikipiki mabasi, daladala mabasi makubwa ili mradi kila kimojawapo kina lake jambo.

SACCOS


Usiwe kama kobe!


Taswira!


PPF tower ya mchwa!

Ghorofa hili limejengwa na mchwa, wadudu hawa wanaushirikiano wa hali ya juu. Siku moja nilibahatika kupita na kuingia nyumba moja kijini na kukuta pamebomolewa kitu mfano wa huo pichani. Nikauliza wakasema ni mchwa hao, na kubomoa tu hakusaidiii maana wanajenga tena, watalamu husema mpaka apatikane malkia wao mchwa ndio wanahama na wenyewe kazi ambayo sio nyepesi kama unavyoifikiria.

Friji la kutumia gesi.

Haya ni mafriji yanayotumika katika mazahanati mengi vijijini kuhifadhia dawa, yanatumia nishati ya gesi hivyo kufanya hata pasipo na umeme kuwepo na huduma hii muhimu.

Fahari ya Mtwara

Hii ndio fahari ya Mtwara, kwa waliowahifika si kitu kigeni. Maendeleo siku hizi ni kwenye chupa kubwa kama makampuni mengine makubwa yanayojulikana.

Mbegu dukani...


Korosho hizooo!


Dawa mseto ya malaria!

Wale wavivu na waoga wa kumeza dawa hii itakuwa kama adhabu kwao.
Ni mseto tuu mpaka unamaliza dozi.

Kokoto nyeupe!


Umewahi kukutana na kokoto za rangi hii?

Tuesday, January 27, 2009

Wanafunzi!!

Kutokana na shule wasomayo ina kaumbali ka kutosha mpaka maeneo wanayoishi, baiskeli huwa ndio usafiri wa haraka kwa wanafunzi hawa.

Linakukumbusha nini hili Trekta?


Video show...


Uwapo kijijini na ukashuhudia kasha la Video kaseti likining'inia kwa mtindo huo linamaanisha kuwa nido picha itayoonyeshwa kenye kaukumbi husika kwa kiingilio cha kati ya shilingi hamsini na mia. Na kikubwa zaidi picha hizo kuwazanakuwa na mtu anaetafsiri iwe ya kihindi nk
Nakushauri siku moja ukiwa kijijini ingia sehemu kama hizo usikie yanayozungummzwa na kutafsiriwa ufe mbavu.