Friday, February 27, 2009

Mambo ya chips na kuku!


Huwezi amini sehemu hii ndio inatoa chips standard kwa wale tuliozoea chips vumbi.
Ukiachilia mbali chips za mahotelini, kwa wakazi wa Mtwara mjini wanapafahamu hapa.

Thursday, February 26, 2009

Kutoka maktaba!


Nyama ya Tembo ikiwa imabanikwa.
Shea hii yote niliuliza nikaambiwa ni kwa ajili ya wanakijiji wa kijiji husika.

Palikuwa hapatoshi!

4WD inaposhindikana hali ndio huwa hivi.

Vipande vya magazeti...

...vipande hivi nya magazeti vimavirigwa tayari kwa kufungi/kuvirigia bidhaa toka dukani kama sukari nk, cha kusikitisha pamoja na mbinu hii mbadala ya urahisi wa kubeba bidhaa husika ni kwamba wakati vinatayarishwa vilikuwa vipo chini kwenye ardhi. Hivyo kiafya inakuwa haijakidhi kisawa sawa kwa namna moja ama nyingine.

Wednesday, February 25, 2009

Dada akisaga Mtama kwa mkono na jiwe!


Mawe ayatumiayo ni yamechongwa kwa mfumo wa duara, halafu kuna mjiti katikati ya tundu la jiwe unafanya lisidondoke/kutoka nje ya mzunguko wakati akilizungusha kusaga mtama huo.

Mweleka baada ya kuseleleka.







Tuesday, February 24, 2009

Kutoka ushauri na maoni mbali mbali

Nianze kwa kuwashukuru mnao nipatia muda wenu na kupita katika blog yangu kuperuzi hili na lile. Lingine lililoniofanya niandike ujumbe huu ni kwamba, baadhi ya wadau kwa namna moja ama nyingine wameomba kuwepo pia picha zinazogusa/zungumzia mazingira na mila pamoja na desturi za huko vijijini nipitako kila kukicha. Jibu nililokuwa nalo la haraka haraka la kueleweka ni kwamba:
Mimi binafsi ni mfanyakazi wa NGO fulani hivyo kupata picha za mila na desturi nk inakuwa ngumu kwa sababu muda wangu mwingi nakuwa bize na kazi inayonipatia ugali.
Pili, sitoweza tumia muda wa kazi kwa kufanya mambo yangu binafsi kwani kazi ni kitu ninachokiheshimu kuliko ugali ninaokula.
Tatu, picha unazozipata (vionjo) unavyovipata ni matokea ya yale ambayo kwa namna moja ama nyingingine nimekuwa nikikutana nayo wakati nikiwa eneo husika, hivyo basi niwaombe radhi kama kuna machache nitakuwa nakunyima kutoka pande za vijijini.
Pamoja na hayo nakutakia siku njema yenye baraka.
Pia nashukuru kama umenielewa maneno yangu.
Wako Mdau.

Taswira

Hiyo myeusi ni mipira itumikayo sana kufungia bidhaa/kitu/mzigo fulani kwa watumiaji wa baiskeli, hali hii ni kutokana ya kwamba kijijini baiskeli ndio njia rahisi ya usafiri wa haraka haraka.

Choice is yours...!!

Asali, mahindi nk bora niuze...

Mwelekeo kwenda kuongeza miti...

Kibanda cha mihogo!

...na uji wa ulezi ukiwa jikoni.

Viatu/Kandambili a.k.a yebo yebo!

Vijijini ndio vinauzika ile mbaya.

Sunday, February 22, 2009

Waijua bandari ya Kilwa Kivinje!

Waswahili wanasema tembea uone!
Kilwa Kivinje mkoani Lindi.

Ukataji miti lipatikane shamba!


Ili kupata shamba mwenye eneo hilo pichani ilimbidi akate kwanza miti ili apate ardhi ya kupanda mazoa yake anayotaraji.

Sauti za Busara zilivyofana!

Shughuli jukwaani (Photo by Blandy)
Palikuwa hapatoshi (Photo by Blandy)
Baada ya shughuli (Photo by Blandy)

Pamoja na ndugu na marafiki tuki-enjoy

Nikiwa na Binamu yangu.
Ndugu na marafiki pia tuki-enjoy.

Kiti cha kamba!

Wengi tumezoea kuona vitanda vya kamba almaarufu "telemka tukaze",
sasa leo nimekuletea kiti chake kwa material yaleyale ya teremka tukaze.

Maji ya mto!

Mto huu ni mpaka kati ya wilaya ya Kilombero na Mahenge mkoani Morogoro.

Neema ya maji bush...

Kwa baadhi ya maeneo vijijini wana neema ya maji safi na salama kama mjini.

Ofisi ya Kata kijijini Mkululu (Masasi-Mtwara)


Ze Taswira


Mashamba ya Chumvi!


Saturday, February 21, 2009

Cheka kiafya!!




Majibu ya post hii ya 23/1/2009 ni haya hapo chini.

Nimebahatika kuona pindi niwapo katika mizunguko yango ya kila siku vijijini kwa gari na kushuhudia nyuma baada ya kupita kwa baadhi ya wanavijiji huchukua wanao wadogo na kwenda kuwakanyagisha zilipoacha/pita alama za matairi ya gari. Nimeshindwa kujua bado mpaka sasa ni nini maana yake!?Wewe una ufahamu wowote juu ya hili?
............................................
Jibu nililolipata ni kwamba,
Wanafanya hivyo kwa mtoto ambae hajaanza kutembea iwe kama kum-wish atembee haraka kwa siku za usoni.
Ndivyo nilivyoambiwa sasa kama ni kweli au la! Hayo ndio majibu

Utamaduni dance!

Hii ndio Africa.
Jivunie kuitwa Mwafrika.

Vijimamboz!

Nikuombe radhi kwa kidogo kutoiona vizuri picha (quality).

Kazi ipo!

Hapa ilikuwa si kazi nyepasi!

Ze taswira.


Siri na raha ya kijijini ni...

...unakuwa na nyumba na uwanja mkuubwa wa kuvinjari na maisha yako.
Hali kama hii huwezi linganisha na wenye nyumba mjini kwa baadhi ya maeneo ya hali ya juu.
Wanasema maisha popote bwana bora kuridhika na ulichonacho.

Tujifunze Kijapani!

Tamka taratibu kwanza usije ukateleza ulimi bure...

Kids from village life


Mikindani beach

Pembezoni kabisa mwa beach ya Mikindani bay (Mtwara)

Friday, February 20, 2009

Lori lililala hapo usiku mmoja!

Hapo ndipo liliponasa kabla ya shughuli ya kulinasua kufanikishwa.

Vijana wakirudisha mzigo wa mbao uliobidi kupakuliwa wote ili lori litoke liliponasa.

Waswahili wanasema ilikuwa "deal" kwa vijana kupata chochote kitu.