Monday, February 9, 2009

Pweza

Kaka pichani akimtayarisha pweza kwa kumpigapiga ili nyama iwe laini.

Juu ya mawe!


Safari na mziki!

Kwa wenzako ni kawaida tu hili. Hapo wanavuka kwenda upande wa pili panaitwa Msangamkuu (Mtwara).
Abiria wakisheheni kuvuka bahari.


Promotion promotion!


Ardhi na utajiri wa Tanzania.

Kama arhi tunayo ya kutoosha nini kingine tupewe?

Mkeka...

Panapo dharula ndege ndogo haitui hapo?

Afya mbele mengine baadae

Pichani kina mama wakingojea kupata tiba/ushauri nk kwa afya za watoto wao.

Ni Jahazi au Mtumbwi?

Binafsi nilijichanganya na kutotambua kama haya niyaonayo ni majahazi au mitumbiwi?
Nisaidie jibu kwa kura yako ya maoni ya jimbo la baharini.

Unawajua Flamingo?


Sunday, February 8, 2009

Duniani!

Maisha hayafanani.

Hili ndilo Tanuli la matofali...

Katika maisha yangu kwa mara ya kwanza Tanuli kama hilo pichani nililifahamia mkoani Mbeya enzi za Sekondari.

Msongamano...

We unadhani walikuwa wanafanya nini hapo?

Kutoka maktaba!


Mshangao...

Watoto hawa niliwakuta wakilishangaa greda wakati wa ujenzi wa barabara, miongoni mwao labda mmoja wao anayo-vision ya kuja kuwa mkandarasi hatuwezi fahamu kwa haraka.

Mnazi mmoja ya Lindi

Upende niliopo mimi ni kutokea wilaya ya Masasi (Mtwara).
Ambapo kulia kwangu ni kuelekea Mtwara na kushoto Lindi.
Na hiki ni kituo cha mizani mnazi mmoja hapo hapo.