Saturday, February 21, 2009

Majibu ya post hii ya 23/1/2009 ni haya hapo chini.

Nimebahatika kuona pindi niwapo katika mizunguko yango ya kila siku vijijini kwa gari na kushuhudia nyuma baada ya kupita kwa baadhi ya wanavijiji huchukua wanao wadogo na kwenda kuwakanyagisha zilipoacha/pita alama za matairi ya gari. Nimeshindwa kujua bado mpaka sasa ni nini maana yake!?Wewe una ufahamu wowote juu ya hili?
............................................
Jibu nililolipata ni kwamba,
Wanafanya hivyo kwa mtoto ambae hajaanza kutembea iwe kama kum-wish atembee haraka kwa siku za usoni.
Ndivyo nilivyoambiwa sasa kama ni kweli au la! Hayo ndio majibu

No comments:

Post a Comment

Be good.