Friday, January 30, 2009

Usafiri wetu kijijini ndio huooo!!

Hali ndio kama hivyo pichani, ukikosa Land Rover almaarufu Muhogo basi utapanda Kenta ama Lori. Ya mjini mjini na kijijini kijijini tu.

Hali halisi kipindi cha mvua...

Watoto hawa nimewakuta wakicheza kwenye maji yaliyotuama ya mvua. Yawezekana shida ya maji vijijini hufanya mpaka hali kama hii ikitokea watoto hawa husherekea. Na wazazi wao sio kwamba walikuwa mbali na watoto hao? Hapana.
Huyu ndie nisema kama kwenye swimming pool basi ndio yupo deep.
Vijimamboz hivyo na patastories.


Mambo yanapokwenda mrama!


Tairi la Lori aina ya fuso likiwa limechomoka na kubakiza nafasi ya fundi kuja kupata ugali wa watoto. Sijajua ni mzigo ulikuwa mzito ama vipi?

Ujenzi huu wa bila mifereji ya maji???

Pichani ni kwamba mkandarasi alipewa kipande cha kukikarabati, lakini kiukweli mifereji ja maji hamna na ndio sababau ya hali kama hiyo pichani. Comment!!

Ukweli kuhusu Prison Break

Prison Break

Ukweli kuhusu Prison Break, imezoeleka masikioni na machoni mwa wengi kuona mitaani Prison Break inapatikana mpaka season eight (8). Hii nathibitisha wazi kuwa Prison Break kihalisia haijafika season eight (8). Hizi mnazoziona mitani ni Episodes tu toka season halali season four (4).

Kwa wanaofuatilia kwa makini watajua ninamaanisha nini. Ukweli ni kwamba kibiashara tu ili kupata pesa wadau Fulani fulani ili wasilale njaa ndio wameamua kuikata kata vipande “episodes” hizo na kuzigawanya katika mafungu wayajuayo wenyewe na kuyaita “season Fulani mpaka Fulani. Ukweli unabaki pale pale kuwa wananchi wamekuwa wakinunua season moja mara nne zaidi bila wao kujua. Ila kutokana na utamu wa sinema yenyewe then watu kwao ni sawa tu bora kuona.

Ilikuwa ni katika kupeana dodoso tu habari ndio hiyo ipo nje nje.


Thursday, January 29, 2009

Ukisikia mkonge ndio huu!!!

Kama inavyoonekana pichani, mkonge wa moja ya gari za kazi Land Cruiser ukiwa umechomewa kwa lengo kuubwa la kupambana na vibaka. Inasemekana gari kama hiyo pindi (Mfano) ipatapo ajali wale wapenda kung'oa vifaa hukimbilia huo mkonge. Habari zinasema kwamba unagharama kuubwa sana ndio sababu ya vibaka kuwinda ulaji huo wanaojua/fahamu magari wanaelewa hilo.

Haya ndio mamboz ya vijijini (Biashara matangazo)


Ufahamu!!

Taa hii inatumia nishati ya umeme wa jua kwa kidhungu Solar power, pamoja na udogo wake inatoa mwanga wa kutosha kama tubelight tulizozizoea majumbani na kwingineko

Football ground.

Pichani unauona uzio ambao upende wa pili kuna mechi ikiendelea wakati picha hii inachukuliwa, kiingilio ndio kitachokuwezesha kujua ya upande wa pili.

Kama mweleka vile...!

Unaweza ukajua nini kimeikumba pikipiki hii?

Kijijini nako kweeema kabisa!

Na njiwa nae yupo kutafuta chakula pichani.

Kwa wengine hili ni "deal" au sio?


Kwenda kwa Rais mstaafu awamu ya tatu...

Unatambaa na mkeka saafi kabisa kwenda kijijini Lupaso (Masasi-Mtwara)
Kituo cha afya kijijini Lupaso hakipo nyuma.

Majengo ya Kitua hicho cha afya Lupaso karibu kabisa na kwa Mheshimiwa rais Mstaafu.



Enzi hizi hata mimi nilipita!!


Nauli!

Inasemekana kuwa kwa baadhi ya magari almaarufu makenta ama malori yabebayo abiria yanayofanya safari zake kwenda Tunduru kupitia njia ya Mtwara wanawake ndio hulipa nauli kubwa, hili nikauliza na kujibiwa kuwa baadhi ya makenta/malori hayo ni vimeo (Mabovu) hivyo linapohitaji msaada wa kulisumkuma liwake wanaume ndio wanashughulika. Swali je kwa mwanaume akitaka kulipa nauli kubwa kidogo na yeye atakubaliwa?