Saturday, February 7, 2009

Ukandarasi!!

Trekta aina ya Valment halipo nyuma katika ujenzi wa barabara, usisahau shambani nako linavuma. Hii ndio hali halisi huku "up-countries" tembea uone.

Chambua picha hizi...

Kwa wabongo unaweza sikia eti hayo maganda ya Madafu deal.

Kuni imezoeleka kuwa deal, ingawa inachangia uharibifu wa mazingira.

Mawe haya yaliyobomolewa toka nyumba za kuishi watu nayo ni deal kwa wengine.

Wewe una lepi?


Eneo nililojidai nalo enzi zetu...

Kwa mkazi wa Dar na kwingineko waliowahi kupasikia Mabibo hostel watakuwa wanajua nazungumzia nini. Ni moja ya Hostel za Chuo Kikuu Dar es Salaam, waliopita hapo hakika watakubaliana na mimi kuwa pana mazingira yanayovutia.

Tudumishe majengo yetu!

Pamoja ya kwamba maghala haya ni ya siku nyingi me napendenzwa nayo kwa jinsi yanavyoboreshwa na kutunzwa. Yapo Mkoani Lindi sehemu inaitwa Mtama.

Gogo njiani!!

Pamoja na kukuta mti huu umeanguka njiani, shukrani kwa wale waliochukua hatua za haraka kusababisha njia iendelee kutumika, vinginevyo hali ingekuwa mbaya zaidi kwa wenye magari.
Pamoja na hayo wadau niliwaona wamejipatia mbao bwerere toka gogo hilo.

Friday, February 6, 2009

Cheka kiafya!!


Mchemsho wa "ngozi ya Mbuzi"

Mimi binafsi nilishangaa, jikoni kunachemshwa ngozi ya Mbuzi na utumbo wake.
Sijui na wewe mwenzangu huu mshamba kama mie kwa kitu hicho pichani?

Ze kufuli...!!




Ukandarasi mteremkoni!!


Picha ya chini inaonyesha mafundi wakimwaga zege kwenye njia iendayo kijiji kimoja kiitwacho Lipalwe kilichopo wilaya ya Tandahimba mkoani Mtwara. Zege hilo linamwagwa mteremkoni kwa ajili ya kipita magari bila matatizo hasa kipindi cha mvua, kama picha ya juu inavyoonyesha zege la awali likiwa bado linadai.

malipo malipo malipo!

Sio malipo ya East Africa no! Hawa ni wakulima wa korosho wakisubiri maliopo yao ya awamu ya pili.
Kama mjuavyo siku hidhi mambo kwa kushirikiana na vyama vya ushirika.

Mchakato wa usafiri vijijini

Bado nitaendelea kukupatia michakato ya usafiri bush.

Baiskeli na vimbwanga...

Kipara cha baiskeli hicho.

Staili hii pichani ngoja nikuchekeshe, kwa hapo sijui jamaa ndio kaipaki au la!!
Ila kuna style kama hiyo panapopaki baiskeli nyiingi hitumika kuibiwa mtu usafiri wake, kwani pindi watapoiweka miguu juu ukija na kuchanganyikiwa huwezi ijua kama ndio yako na ukipoteza netwrok tu umeenda na maji tena ya mafuriko. Wameibiwa wengi sana kwa style hiyo Mtwara.


Soma hii...!


Sheli ya mafuta bush...!!


Haya ndi mambo ya vijijini usishangae sana.

Mjini ipo hii?

Huyu ndie mfano wa baba anaejali, ameamua kumleta mwanae mwenyewe zahanati.