Friday, February 6, 2009

Cheka kiafya!!


Mchemsho wa "ngozi ya Mbuzi"

Mimi binafsi nilishangaa, jikoni kunachemshwa ngozi ya Mbuzi na utumbo wake.
Sijui na wewe mwenzangu huu mshamba kama mie kwa kitu hicho pichani?

Ze kufuli...!!




Ukandarasi mteremkoni!!


Picha ya chini inaonyesha mafundi wakimwaga zege kwenye njia iendayo kijiji kimoja kiitwacho Lipalwe kilichopo wilaya ya Tandahimba mkoani Mtwara. Zege hilo linamwagwa mteremkoni kwa ajili ya kipita magari bila matatizo hasa kipindi cha mvua, kama picha ya juu inavyoonyesha zege la awali likiwa bado linadai.

malipo malipo malipo!

Sio malipo ya East Africa no! Hawa ni wakulima wa korosho wakisubiri maliopo yao ya awamu ya pili.
Kama mjuavyo siku hidhi mambo kwa kushirikiana na vyama vya ushirika.

Mchakato wa usafiri vijijini

Bado nitaendelea kukupatia michakato ya usafiri bush.

Baiskeli na vimbwanga...

Kipara cha baiskeli hicho.

Staili hii pichani ngoja nikuchekeshe, kwa hapo sijui jamaa ndio kaipaki au la!!
Ila kuna style kama hiyo panapopaki baiskeli nyiingi hitumika kuibiwa mtu usafiri wake, kwani pindi watapoiweka miguu juu ukija na kuchanganyikiwa huwezi ijua kama ndio yako na ukipoteza netwrok tu umeenda na maji tena ya mafuriko. Wameibiwa wengi sana kwa style hiyo Mtwara.


Soma hii...!


Sheli ya mafuta bush...!!


Haya ndi mambo ya vijijini usishangae sana.

Mjini ipo hii?

Huyu ndie mfano wa baba anaejali, ameamua kumleta mwanae mwenyewe zahanati.

Thursday, February 5, 2009

Kazi ya watoto ukutani...!!


Mkaa sokoni

Nunua na kiroba chake au unabadilishana na kiroba kingine, ndio biashara.

Tandahimba saaafi kabisa.



Pichani ni majengo mapya ya Hospitali ya wilaya ya Tandahimba (Mtwara) yakiwa katika hatua ya mwisho kabisa. Kazi kwao wananchi siku za usoni kuyatunza.


Pata hii kwenye maelezo...

Pichani sikuweza kuwapata wote ila ni baadhi ya vijana wakiwa chini ya mti majira ya saa tatu asubuhi. Hii nimeishuhudia sana vijijini mkoani Mtwara kwa vijana kulundikana vijiweni wakati wa kazi. Sio kwamba ardhi haipo ya kujishughulisha! Hapana jibu ni ipo, hiyo ndio hali kalisi.

Niwapo vijijini hii ndio pasi


Ukiwa kijijini huwezi kuikwepa hii, ingawa hata mijini wapo wanaozitumia mapaka leo.